Siku moja nilienda bank kwa ajili ya kufungua account, siku hiyo nilipanga kumaliza kila kitu kinachohusiana na kufungua account hiyo maana nilikuwapo katika bank hiyo siku mbili tofauti za nyuma kwa ajili ya kushughulikia account hiyo bila mafanikio.

          Siku hiyo nilitoka nyumbani kwa kusudi moja tu la kuhakikisha nimefanikiwa kufungua account,maana nilibeba kila ambacho kingehitajika kuifungua account hiyo,tofauti na nilivyozoea kukuta watu wachache na kupata huduma haraka, siku hiyo watu walikuwa wengi na mhudumiaji counter alikuwa mmoja tu;nilibadilisha mapozi yote ya ukaaji na usimamaji ili kuvuta muda kwa ajili ya kupata huduma,nilisubiri na kusubiri nakusubiri bila mafanikio yoyote,

          Nilifika pale asubuhi mida ya saa nne lakini mpaka wanakula chakula cha mchana mimi bado nipo tu,mpaka inaanza kuingia saa tisa mimi bado nipo tu…jambo moja nakumbuka nilijiambia ni kwamba  “leo siondoki mpaka nimekamilisha zoezi hili”

          Kuna wakati ilionekana kama sitaweza kufanikiwa kufungua account ile kwa sababu za kisheria, ulianza mjadala wa sheria inasemaje juu ya uanzishwaji na uendeshaji wa account ile niliyokuwa naitaka,mara zote nilikuwa na kicheko moyoni nikijua fika kwamba sijawahi kutumia muda wangu namna hii halafu nikashindwa,moyoni mwangu niliamini kabisa kwamba ningeweza kupata huduma ile na kukamilisha siku hiyohiyo.

          Baada ya yote hayo, wakati inaelekea saa kumi faili langu likaanza kushughulikiwa kwa haraka maana hata watu walikuwa wamepungua,kwakufupisha stori ni kwamba  nilifanikiwa kufungua account ile na kuanza kuweka pesa siku hiyo hiyo kama ilivyohitajika.

          Ikawa siku nyingine tena Wakati nikiwa kwenye basi la mwendo kasi nikiwa natokea posta mida ya saamoja jioni, nikiwa kwenye basi, kuna kituo basi lilisimama ili kuchukua abiria hali ya kuwa basi lilikuwa limejaa sana,  baadhi ya abiria walianza kulalamika kwamba dereva asifungue mlango maana basi lilijaa sana, wakati dereva akiwa amefungua milango na watu kuanza kuingia hivyohivyo nilibahatika kumuona mama mmoja ambaye alionekana kungangana kuingia japokuwa mwanaume mmoja aliyesimama mlangoni alionekana kabisa kumpinga asiingie kwa kumuwekea kikumbo na kumsukumizia nje…kwakuwa mimi nilikuwa karibu na Yule kaka niliona mchezo mzima unavyoendelea,chakushanganza ni kwamba niliona Yule mama akiendelea kungangania gari lile na hatimae wakati gari linaanza kuondoka na yeye alikuwa mmoja wa wasafiri tuliokuwa nao.

          Kuna kitu cha kujifunza kutoka katika habari hizi mbili ambazo zinatukumbusha kile alichosema Yesu kwenye Biblia kwamba atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokoka,
Swali langu kwako leo ni ,Je umeweza kuvumilia pale ulipoona kama ndoto yako inafifia, uliendelea kukazana kupambana maono yako yathibitike au uliachia ngazi na kukata tamaa?

          Nakukumbusha leo kuendelea kupambana mpaka tone la mwisho kuhakikisha unafikia mwisho mwema ulioandaliwa na Mungu,usikate tamaa njiani,Be strong.

Anza sasa.

Maoni

  1. Hii ni kweli kabisa, na nimeiona inatokea kwangu mara nyingi sana.
    Ukivumilia mpaka mwisho utapata unachotaka.

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUFANIKIWA KIMAISHA.