KUFANIKIWA KIMAISHA.

                                                      MAFANIKIO YA KIMAISHA

Ili maisha yangu yawe vile Mungu anataka niwe imenipasa kuwa na nidhamu, kuna maeneo kadhaa ambayo napaswa kuweka bidii ya nidhamu katika hayo,maeneo kama;Mahusiano na Mungu,muda,pesa pamoja na kazi ni vitu ambavyo lazima niviangalie kwa jicho la pekee ukizingatia kwamba ni maeneo nyeti yatakayonipelekea kufikia malengo kama nikiyatendea kwa ustadi.
Kama alivyosema kaka Fela Duratoye katika moja ya semina alizokuwa mzungumzaji juu ya jinsi ya kwenda mbele kwa kasi,alisema inabidi mtu aone ni jinsi gani anaweza kuona vitu vya;
·         Kuanza kufanya
·         Kuacha kufanya
·         Kufanya zaidi
·         Kupunguza kufanya.
            Ili ufanikiwe kimaisha ni jambo la busara kujua ni mambo gani ya kuyaanza, yapi ya kuyaacha na pia yapi ya kufanya zaidi na yapi ya kupunguza kufanya.
Duniani kuna mambo mengi, bila  kuwa makini unaweza kujikuta unajihusisha na kila kitu haliyakuwa muda ulionao ni mchache,mwisho wa siku unajikuta umefanya mambo mengi lakini hayana faida yoyote sio tu kwako bali na kwa jamii inayokunzunguka,Itambulike wazi kuwa kila mtu aliyezaliwa mara ya pili ni nuru,kwa lugha rahisi kila aliyezaliwa mara ya pili ni suluhisho la tatizo Fulani,
            Kuokoka pekee hakutoshi,lazima ukue na kujua sababu ya wokovu wako ndivyo ilivyo na kuzaliwa,kuzaliwa pekee hakutoshi,lazima ufike mahali pa kujua kwanini umezaliwa ili uanze kuiishi kwa ukamilifu sababu ya kuzaliwa kwako.
Nilisoma mahali mwanafalsafa mmoja aliandika kuwa dunia ni ya ajabu sana si kwasababu ya watu wanaotenda maovu bali ni ya ajabu kwa sababu ya watu wanaowatazama wanaotenda maovu na kuwaacha hivyohivyo.
            Je kuna jambo la msingi ambalo mpaka unaingia kitandani leo unaweza kusema kuwa umelifanya? Kuna watu wa aina mbili huku Duniani,
  •     Wanaofanya vitu vitokee
  •  Wanaotazama vitu vikitokea.

Wewe upo katika kundi gani kati ya hayo mawili tajwa hapo juu? Kama haufanyi mambo yatokee ujue tayari unaingia kundi la wanaotazama yanayotokea, huu sio wakati wa kujifariji, huu ni wakati wa kuonesha ulimwengu kuwa umekataa kufa na lulu uliyokujanayo huku duniani,
            Utajisikiaje kama siku unaingia mbinguni na kuoneshwa picha ya ulivyotegemewa kuwa na uneshindwa kuwa na ukaoneshwa namna ambayo ungeweza kabisa kufikia kusudi la kuumbwa kwako katikati ya changamoto ulizokuwa unapitia; amua leo kuishi vile ulivyokusudiwa kuishi huku chini ya jua,Maisha ya kifalme na kikuhani.
Kama ningeambiwa kufupisha ujumbe huu kwa maneno mawili ningekwambia;

                                                     #ANZASASA.


Maoni

  1. Ukishajua umekuja duniani kufanya nini,anza kufanyia kazi.

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii